Mbunge wa Mikumi kupitia CHADEMA ambaye pia ni msanii mkongwe wa bongo
fleva Prof Jay, kwa Mara ya kwanza ametoa ya moyoni baada ya nyumba yake
kubomolewa na TANROADS
Kwenye ukurasa wake wa instagram Prof Jay ameandika ujumbe akisema amejifunza kumshukuru Mungu, huku akuonyeshwa kushangazwa na kitendo cha serikali kutoheshimu uamuzi wa mahakama kama mhimili wa nchi.
"Sijawahi kuumia kiasi hiki, nimesikitishwa sana jinsi Tanroads wanavyoweza kujichukulia maamuzi bila ya kujali mhimili muhimu wa Mahakama wametoa maagizo gani. Na taratibu zilizotumiwa kubomoa nyumba yangu bila ya mimi na Tanesco kupewa taarifa saa kumi na mbili jioni (haukuwa muda wa kazi) na kubomoa huku umeme ukiwa unawaka ni kitendo ambacho kwanza kina hatarisha maisha ya wabomoaji wenyewe, maisha ya familia yangu pamoja na majirani zangu , limenisikitisha zaidi", ameandika Prof. Jay.
Kwa mujibu wa Prof Jay nyumba yake imebomolewa Septemba 29,2017, na hakufanikiwa kuokoa kitu chochote ambacho kilikuwemo.
Kwenye ukurasa wake wa instagram Prof Jay ameandika ujumbe akisema amejifunza kumshukuru Mungu, huku akuonyeshwa kushangazwa na kitendo cha serikali kutoheshimu uamuzi wa mahakama kama mhimili wa nchi.
"Sijawahi kuumia kiasi hiki, nimesikitishwa sana jinsi Tanroads wanavyoweza kujichukulia maamuzi bila ya kujali mhimili muhimu wa Mahakama wametoa maagizo gani. Na taratibu zilizotumiwa kubomoa nyumba yangu bila ya mimi na Tanesco kupewa taarifa saa kumi na mbili jioni (haukuwa muda wa kazi) na kubomoa huku umeme ukiwa unawaka ni kitendo ambacho kwanza kina hatarisha maisha ya wabomoaji wenyewe, maisha ya familia yangu pamoja na majirani zangu , limenisikitisha zaidi", ameandika Prof. Jay.
Kwa mujibu wa Prof Jay nyumba yake imebomolewa Septemba 29,2017, na hakufanikiwa kuokoa kitu chochote ambacho kilikuwemo.
No comments:
Post a Comment